GAIDI WA DAESH AKAMATWA NCHINI IRAN.

Shirika la habari AhlulBayt (a.s) ABNA: Kamanda wa jeshi la Iran katika mji wa Shahriar ametangaza kukamatwa kwa gaidi mmoja wa kikundi cha kigaidi cha Daesh katika sehemu ya Andisheh na amesisitiza kwa kusema kuwa kikundi cha kigaidi cha Daesh kilikuwa kinajipanga kwa kufanya matukio ya kigaidi ndani ya mwezi wa Muharram katika mji wa Teheran.
Hayo yamesemwa na kanali (Amini Yaminiy) alipokuwa amekutana na vyombo vya habari na kubainisha kuwa: mmoja kati ya magaidi wa Daesh tumemkamata sehemu iitwayo Andisheh katika mkoa wa Shahriar.
Aidha amebainisha kuwa kikundi cha kigaidi cha Daesh kilikuwa kimepanga kufanya mashambulio 300 ya kigaidi katika mwezi wa Muharram ndani ya mji mkuu wa Teheran, ambapo mpaka sasa tumepata ripoti nyingi kuhusu matukio hayo kupitia simu ya gaidi huyo na bado tunaendelea kumuhoji.

DONATE FOR MASJID IMAM ALI (A.S)

 

UTAWALA HARAMU WA ISRAEL WAENDELEA KUUZA SILAHA NCHINI BURMA.


Nchi ya Israel ipo katika tuhuma nzito kutoka ka mashirika ya kutetea haki za binaadamu, kwa kitendo chake cha kuendelea kuizuia silaha jeshi la nchi ya Burma mbali na mauaji dhidi ya jamii ya Waislam walio wachache katika nchi hiyo.
Uchunguzi wa mashirika ya kupigania haki za binadamu umebaini kuwa zaidi ya vifaru vya kijeshi 100, pamoja na merikebu na silaha nyingine ndogondogo, zimeuzwa kwa serikali ya Burma na makampuni ya kiisareli.

Kampuni moja la kiislaeli liitwalo TAR Ideal Concepts, ambalo limekuwa likitoa mafunzo ya kwa vikosi maalumu katika jimbo la kaskazini la Rakhine. Jimbo hilo ndilo ambalo mauaji yanafanyika llimeweka picha katika mtandao ukiwaonesha wafanyakazi wake wakitoa mafunzo ya kivita na namna ya kushikilia silaha.
Nchi za ulaya EU pamoja na Marekani ziliiwekea vikwazo nchi ya Burma vya kuiuzia silaha vikwazo ambavyo bado vinafanya kazi.
Ofer Neiman mwanaharakati wa haki za binaadamu amenukuliwa na shirika la habari la Middle East Eye akisema “Serikali imekuwa ikiiuzia silaha jeshi la kidikteta la Burma kwa miaka mingi sasa”.
Picha za watoto wakiwa wamekatwa vichwa na vijiji kuteketea kwa moto kulikofanywa na jeshi la Burma zimeenea duniani kote.

chanzo cha habari: www.Independent.co.uk

BHRN: SIO WAISLAMU WA RAKHINE TU WANAOUAWA MYANMAR.




Shirika moja la kutetea haki za binadamu nchini Myanmar limetoa ripoti iliyofichua kuwa Waislamu katika maeneo yote ya nchi hiyo wanauawa na kuhujumiwa na wanajeshi wa nchi hiyo na sio wa kabila la Rohingya tu katika mkoa wa Rakhine.
Ripoti iliyotolewa jana Jumanne na Burma Human Rights Network imesema kuwa, serikali inawaunga mkono wanajeshi na mabudha wenye misimamo mikali kuwashambulia Waislamu katika kila pembe ya nchi hiyo ya mashariki mwa bara Asia.
Ripoti hiyo imesema kuwa, mbali na Waislamu wa Myanmar kunyimwa huduma za msingi kama matibabu wanapokwenda hospitalini, lakini pia serikali imekataa katakata kuwapa vitambulisho vya taifa.
Ripoti ya Burma Human Rights Network imebainisha kuwa, Waislamu katika miji na vijiji 46 nchini Myanmar wanapitia kila aina ya jinai kutoka kwa askari wa jeshi la nchi hiyo wakishirikiana na Mabudha wenye misimamo mikali.
Tangu tarehe 25 Agosti mwaka huu, jeshi la Myanmar kwa kushirikiana na Mabudha wenye misimamo mikali limekuwa likiwashambulia Waislamu wa jimbo la Rakhine, ambapo zaidi ya 400 miongoni mwao wamekwishauawa, huku wengine zaidi ya laki 1 na 25 elfu wakikimbilia Bagladesh.
Mauaji na jinai hizi zinafanyika mkabala wa kimya cha taasisi husika za kimataifa kama vile Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.



KUENDELEA KUULIWA WAISLAMU WA ROHINGYA NCHINI MYANMAR.
Wawakilishi wa bunge la Myanmar wametaka kujengwa vijiji zaidi vya kikabila kwa lengo la kuwakandamiza Waislamu wa jamii ya Rohingya ikiwa ni katika kuendelea kuangamizwa kizazi cha Waislamu hao huko Myanmar khususan katika mkoa wa Rakhine.
Aghalabu ya Waislamu wa Rohingya wanaishi katika mkoa huo unaopatikana magharibi mwa Myanmar. Pamoja na kuwepo mkakati wa kuwafukuza Waslamu wa Rohingya katika mkoa wa Rakhine, wabunge wa Myanmar wanakiri kuwa tangu maelfu ya miaka nyuma, eneo hilo limekuwa makazi asilia ya Waislamu wa Rohingya tangu enzi za mababu likijulikana kwa jina la Aragan, na vile vile lilikuwa na utawala wa kifalme kwa muda wa miaka mia tatu. Hata hivyo mashinikizo dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya yalianza rasmi katika muongo wa sitini miladia baada ya kuingia madarakani wanajeshi nchini humo; na kisha mashinikizo hayo kuendelezwa kufutia vitisho na uchochezi wa watawala wa Kibudha wenye misimamo mikali kama Ashin Wirathu. Kwa kadiri kwamba kuanzia mwaka 2012 Waislamu wa Rohingya zaidi ya elfu moja waliuawa na wengine zaidi ya laki moja kulazimishwa kuwa wakimbizi katika nchi jirani kutokana na ukandamizaji na mauaji ya umwagaji damu yanayofanywa na Mabudha wenye misimamo ya kufurutu ada.
Wawakilishi wa bunge la Myanmar wametaka kujengwa vijiji zaidi vya kikabila kwa lengo la kuwakandamiza Waislamu wa jamii ya Rohingya ikiwa ni katika kuendelea kuangamizwa kizazi cha Waislamu hao huko Myanmar khususan katika mkoa wa Rakhine.
Aghalabu ya Waislamu wa Rohingya wanaishi katika mkoa huo unaopatikana magharibi mwa Myanmar. Pamoja na kuwepo mkakati wa kuwafukuza Waslamu wa Rohingya katika mkoa wa Rakhine, wabunge wa Myanmar wanakiri kuwa tangu maelfu ya miaka nyuma, eneo hilo limekuwa makazi asilia ya Waislamu wa Rohingya tangu enzi za mababu likijulikana kwa jina la Aragan, na vile vile lilikuwa na utawala wa kifalme kwa muda wa miaka mia tatu. Hata hivyo mashinikizo dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya yalianza rasmi katika muongo wa sitini miladia baada ya kuingia madarakani wanajeshi nchini humo; na kisha mashinikizo hayo kuendelezwa kufutia vitisho na uchochezi wa watawala wa Kibudha wenye misimamo mikali kama Ashin Wirathu. Kwa kadiri kwamba kuanzia mwaka 2012 Waislamu wa Rohingya zaidi ya elfu moja waliuawa na wengine zaidi ya laki moja kulazimishwa kuwa wakimbizi katika nchi jirani kutokana na ukandamizaji na mauaji ya umwagaji damu yanayofanywa na Mabudha wenye misimamo ya kufurutu ada.
Utekelezaji wa mauaji au maangamizi ya kizazi ya Waislamu wa kabila la Rohingya umebadilika na viongozi wa serikali na wale wa kieneo wameazimia kuasisi vijiji vya kikabila ili kuwanyang'anya ardhi jamii hiyo kwa kuzingatia radiamali inayotolewa na jamii ya kimataifa kwa mauaji ya kizazi huko Myanmar na pia kuwahusu viongozi wa nchi hiyo khususan Aung San Suu Kyi, kiongozi wa chama tawala cha National League for Democracy (NLD) ambaye pia ni mshauri wa ngazi ya juu wa serikali ya nchi hiyo. Siasa hizo zinafuatliliwa kwa jadi na kupewa kipaumbele cha awali na wabunge wa Myanmar ambao wengi ni kutoka chama cha National League for Democracy chini ya uongozi wa Bi Suu Kyi. Jenerali Than Htut Naibu Waziri Anayehusika na Masuala ya Mipaka wa Myanmar amesema kuwa vijiji 36 vya kikabila vimejengwa katika maeneo tofauti mkoani Rakhine na kwamba serikali ina mpango wa kuyahamisha makabila mbalimbali kutoka katika eneo la Yangon na kuyapeleka katika maeneo hayo lengo likiwa ni kuvuruga muundo wa kijamii wa mkoa wa Rakhine na hivyo kuwadhihirisha Waislamu wa Rohingya kuwa ni jamii ya waliowachache. Kuanzia mwezi Oktoba mwaka 2016 hadi Februari mwaka huu maeneo ya Buthidaung na Mandau katika mkoa huo yamekumbwa na mashambulizi ya umwagaji damu ya Mabudha wenye misimamo mikali dhidi ya Waislamu wa Rohingya.

Kwa kuzingatia nafasi nzuri ya kijiografia ya mkoa wa Rakhine kwa upande wa hali ya hewa na ardhi ya kilimo na vile vile shughuli za kibishara, ni karibu miongo sita sasa ambapo Mabudha wenye misimamo mikali wameanzisha jitihada kubwa kwa kutumia mbinu mbalimbali za kiuongozi na kijeshi ili kupora na kumiliki ardhi, vituo vya kibiashara na kuwadhibiti Waislamu wa Rohingya; ambapo lengo lao kuu ni kuwafukuza katika makazi na nyumba zao kwa kutekeleza mauaji ya kizazi dhidi ya jamii hiyo. Pamoja na hayo yote, kusimama kidete na kuendesha muqawama Waislamu wa kabila la Rohingya mkabala na mashinikizo na ukandamizaji wa Mabudha wenye misimamo ya kuchupa mipaka huko Myanmar kumekwamisha kutekelezwa siasa za kuangamiza kizazi dhidi ya jamii hiyo iliyodhulumika; na hilo ndilo limewafanya watawala wa nchi hiyo wakimbilie kuasisi vijiji vya kikabila ambavyo hakuna matarajio kwamba vitaweza kufanikisha mkakati wao wa kuwafukuza Waislamu wa Rohingya katika ardhi zao asilia. http://parstoday.com/…/world-i30216-kuendelea_kuuliwa_waisl…





KAMPENI YA "NIMR HATASAHAULIKA", YAANZA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII SAUDI ARABIA.


Wanaharakati wa Saudi Arabia wameanzisha kampeni iliyopewa jina la "Nimr Hatasahaulika" katika harakati ya kumkumbuka na kumtetea mwanazuoni mashuhuri wa nchi hiyo Sheikh Nimr Baqir al Nimr aliyeuawa na utawala wa kifalme wa Saudia mwaka jana wa 2016. Wanaharakati hao pia wamewataka wanaharakati wenzao kuunga mkono kampeni hiyo.
Sheikh Baqir Nimr alitiwa nguvuni mwezi Julai mwaka 2012 kufuatia maandamano na malalamiko makubwa ya kudai haki na uadilifu ya watu wa eneo la Qatif mashariki mwa Saudi Arabia lenye Waislamu wengi wa madhehebu ya Shia. Tarehe 15 Oktoba mwaka 2015 Sheikh Nimr alihukumiwa kifo kwa kukatwa kichwa kwa panga na kusulubiwa kadamnasi kwa tuhuma ambazo hazikuwa na msingi eti za kuhujumu usalama wa taifa na kupiga vita utawala wa nchi hiyo. Hukumu ya kifo dhidi ya msomi huyo wa Kiislamu na wenzake 46 waliotambulishwa kuwa ni magaidi, ilitekelezwa tarehe 2 Januari 2016 na kulaaniwa na mataifa ya Kiislamu, nchi na jumuiya mbalimbali za kutetea haki za binadamu.
Mtaalamu wa masuala ya haki za binadamu wa Bahrain, Baqir Darwish anasema: "Kadhia ya kuuliwa shahidi Sheikh Nimr Baqir al Nimr ilikuwa mtihani mkubwa kwa jamii ya kimataifa. Inasikitisha kwamba, jamii ya kimataifa ilifeli katika mtihani huo kwa kushindwa kuzuia mauaji ya msomi huyo wa Saudia na iliupatia zawadi utawala wa Aal Saud kwa kutenda jinai hiyo", mwisho wa kunukuu.
Utawala wa kifalme wa Saudia umezidisha mashinikizo na ukandamiza dhidi ya raia wa nchi hiyo hususan Waislamu wa madhehebu ya Shia, na jeshi la nchi hiyo kwa sasa linafanya mashambulizi makali zaidi kuwahi kushuhudiwa dhidi ya Mashia wa mashariki mwa nchi hiyo. Pamoja na hayo malalamiko yanayoendelea kufanywa na Wasaudia dhidi ya jinai ya kumuua shahidi Sheikh Baqir Nimr ni kielelezo kwamba, ukandamiza huo si tu kwamba umezima na kupunguza malalamiko na upinzani wa wananchi, bali pia umeyapanua zaidi hadi kwenye mitandao ya kijamii.
Licha ya mbinyo na ukandamizaji huo dhidi ya wapinzani nchini Saudia, harakati za kudai uadilifu zinazidi kuongezeka kila siku, suala linaloonesha kwamba, vitisho, mauaji na kufungwa jela havijafanikiwa kuzima sauti na harakati za kupigania haki, uhuru wa kuabudu na demokrasia. Itakumbukwa kuwa, Sheikh Baqir al Nimr pia alisimama kidete hata alipokuwa katika jela za utawala wa kifalme wa Saudi Arabia na hakusalimu amri hadi alipouliwa. Kuendelea kwa upinzani na malalamiko hayo ya wananchi licha ya ukatili na mauaji hayo kuna maana kwamba, watu wa Hijaz wameazimia ipasavyo kwa ajili ya kutimiza malengo yao na kuuondoa utawala wa kidikteta na kidhalimu unaotawala nchi hiyo.
Ali Raslani ambaye ni mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu wa Lebanon anasema: "Licha ya kupita karibu mwaka mmoja na nusu tangu kuuawa shahidi Sheikh Nimr Baqir al Nimr tunaona kuwa, msomi huyo anakumbukwa mahala pote, na roho yake ya kupambana na sera za kuwatenganisha Waislamu na kukabiliana na dhulma zinazitia hofu tawala za watenda jinai".

HARAKATI ZA UJENZI WA MSIKITI ZINAENDELEA.

Ujenzi wa Msikiti unaendelea katika Mkoa wa Tanga Wilaya ya Lushoto hii ni moja ya jitihaga za kufanikisha jamii zetu zinaishi katika sehemu salama na kujipatia elimu yenye manufaa kwa ajili ya kukuza uelewa juu ya maadili yanayotakiwa kwa Mwanadamu.

WANAHARAKATI WA DINI YA KIISLAM WAUNGANA TANGA WILAYA YA LUSHOTO.


Wanaharakati wa dini ya Kiislam wameungana katika Mkoa wa Tanga Wilayani Lushoto kwa ajili ya kuendesha harambee maalumu kwa ajili ya Msikiti ambao umechukua mda mrefu bila kufanyiwa matengenezo sasa Wanaharakati hao wameamua kuchukua fursa ya kuutengeneza kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wa dini Tukufu ya Kiislam.

MAELFU YA WAIRAN WAJITOKEZA KATIKA MAZISHI YA MASHAHIDI.


















Maelfu ya wa Iran wamejitokeza katika mazishi ya Mashahidi waliokufa katika mashambulizi ya kigaidi.
Wiki iliyopita siku ya Jumatano jiji la Tehran lilikumbwa na mashambulizi kadhaa ya kigaidi. Watu kadhaa waliokuwa na silaha asubuhi ya jana waliingia katika majengo ya Bunge la Iran ambapo walikabiliwa na jibu kali la askari walinzi wa eneo hilo.
Watu kadhaa waliuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa.
Sambamba na shambulizi hilo, magaidi wengine wanne walifyatua risasi ovyo katika haram ya Imam Khomeini kusini mwa jiji la Tehran ambako waliua mtu mmoja na kujeruhi wengine wanne. Gaidi mmoja alijilipua kwa bomu baada ya kukabiliwa na hujuma kali ya askari usalama, mwingine aliuuawa kwa kupigwa risasi, na gaidi mwenzao wa kike ametia nguvuni baada ya kujeruhiwa na askari usalama. Magaidi wengine kadhaa wametia nguvuni kabla ya kutekeleza uhalifu. Kundi la kigaidi la Daesh limetangaza kuwa ndilo lililotekeleza mashambulizi hayo.

DOKTA ALI LARIJANI: KUWAJULIA HALI WAHANGA







Spika wa Bunge la Iran Dakta Ali Larijani amewatembelea wahanga walioshambuliwa na Magaidi siku ya Jumatano nchini Iran.