Mwaka 1994 mimi niliamua kuwa Shia Ithna
Asharriyah na wenyeji wangu walionipokea ni Bilal Muslim Mission of
Tanzania chini ya uongozi wa Maulana Akhtar Rizivi na utendaji wa Mzee
Fidah Husain Hameer. Ombi langu la kwanza kwao ili niwe Mwanaharakati
mzuri wa Madhehebu ya Ahlul Bayt (a.s) nijengewe Msikiti mjini Lushoto
ambapo ndipo mimi kwa miaka karibu 15 nilifanikiwa kueneza
Uwahhabi(Answaru Sunna) Wilaya yote ya Lushoto. Na nilifanikiwa kujenga
misikiti isiopungua 10 chini ya African Muslim Agency. Mimi nilikuwa
msitari wa mbele katika mapambano na madhehebu ya Sunni (Madhehebu ya
Shafii) ambayo ndio yaliyokuwa Wilaya ya Lushoto na Tanga yote kwa
jumla. Katika Tanzania yote kwa ujumla chini ya vijana wa Warsha ya
Waandishi wa Kiislamu tulifanikisha kuanzisha Seminari za Kiislamu,
nikiwa Kiongozi wa Idara ya D’awa, nilisimama mahakamani mwaka mzima kwa
niaba ya Warsha ya Waandishi wa Kiislamu kuishitaki Wizara ya Elimu na
BAKWATA kwa kuwanyima Waislamu wasiwe na Seminari zao wakati Wakristo
wanazo. Kesi hiyo tulishinda na Masjid Qubah ikiwa Seminari ya kwanza
Tanzania bila kuwa chini ya BAKWATA. Ushindi wa kesi hiyo ukafungua
milango kwa Waislamu wakawa na Seminari zao. Almuntaziri ikiwa moja
wapo. Kwa msingi huo tulikubaliana tujenge msikiti Lushoto mjini lakini
kiwanja kiwe kwa jina la Rejesterd Trustees of Bilal Muslim Mission of
Tanzania. Mimi nilitafuta kiwanja baada ya kukosa nilikubali kutoa
kiwanja changu kilichoko mjini Lushoto (Wakfu) kwa Bilal Muslim Mission
of Tanzania ili mradi tuwe na msikiti mjini. Insha’allah tutaendelea
kuwapatia historia ya Mwanaharakati huyu mkongwe