LINI WAPALESTINA WATAKUWA UHURU NA ARDHI YAO.



Ni kwa mda gani ulimwengu utaziba masikio yake ili usisikilize umwagaji damu wa Wapalestina mikononi mwa wavamizi? Je! Wapalestina hawapaswi kufurahia haki yao ya kuishi kwa uhuru katika ardhi yao kama watu wengine ulimwenguni? Uhalisi wa kimataifa ambao kwamba tulilinganiwa na ulimwengu kuutambua na kushikana nao unakanyagwa kila siku katika Palestina na jeshi la wavamizi na ongezeko lake la kijeshi na mazingira yanayowekwa katika miji yao, vijiji, kambi, na kusababisha umwagaji wa damu wa Wapalestina kwa mashine pofu za kijeshi zilizokusudiwa kwa ajili ya kuwaangamiza Waislamu na wasio Waislamu katika ardhi ya Palestina pamoja na Masjid Al- Aqsa.