WAUMINI WA MADHEHEBU YA SHIA ITHNA ASHARIYYA JIJINI DAR ES SALAAM WAMESWALI SWALA YA EID FITR KATIKA KIWANJA CHA PEOPLE KILICHOPO KIGOGO POST.

Swala ya Eid Fitr iliyoswaliwa Kigogo, jijini Dar es Salaam. Imam wa swala ya Eid Sheikh Hemed Jalala amewataka Viongozi wa dini kutoruhusu sehemu za ibada kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani nchini pia imam huyo ameyalaumu mataifa makubwa kwa kunyamazia mauwaji yanayoendelea hivi sasa Palestina mwisho amesema matukio yanayotokea hivi sasa katika nchi ya Nigeria ni njama za kutaka kuizima harakati ya Kiislamu inayosimamiwa na Sheikh Ibrahim Zakyzaky, ameendelea kwa kusema kikundi cha Boko haramu ni kikundi kilichotengenezwa kwa ajili ya kupambana na harakati ya kweli iliyopo katika nchi hiyo kwani siku zote mkweli uondolewa, Sheikh Hemed Jalala ametoa salamu za pole kwa kiongozi wa harakati ya Kiislamu Sheikh Ibrahim Zakyzaky kutokana na msiba mkubwa aliyoupata.