MAADHIMISHO YA QUDS YAFANYIKA KIGOGO, JIJINI DAR ES SALAAM.


Alhamdulillah siku ya leo tumeimaliza kwa kufanya matembezi ya kupinga ukandamizaji dhidi ya wanadamu ulimwenguni, matembezi hayo yamefanyika Kigogo jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuwaunga mkono wanaharakati wa Palestina ambao wanaipigania ardhi yao, baadhi ya Wanaharakati wa Kiislamu wenye misimamo thabiti walijitokeza katika matembezi hayo ya kuwaunga mkono wapambanaji hao wa Palestina kwa mavazi ya fulana zenye picha za Viongozi wa Moqawama (Hizbollah) na Masjid Al-Aqsa na wengine walibeba mabango yenye jumbe mbali mbali pamoja na picha za wahanga wa Palestina cha hajabu na kusikitisha baadhi ya VOLUNTEER na viongozi wa matembezi hayo walizuia athari za Moqawama kwa kuhofia kuonekana wanaunga mkono makundi ambayo Marekani na washirika wake wameyaweka katika orodha ya magaidi ulimwenguni Viongozi hao na VOLUNTEER wanadai kuonekana katika jamii athari za Moqawama kutaleta matatizo na picha mbaya katika harakati zetu, sisi kama wanaharakati wa Kiislamu na VIjana wa Kiislam tumesikitishwa sana kuona baadhi ya VOLUNTEER wakimsukuma mtu kutoka meza kuu alipokuwa akichukua habari na wengine kuvuliwa fulana zao kwa kua wamevaa fulana zenye picha za Maulamaa ambao Mwaamerika anaitakidi kuwa ni magaidi kwa kweli kitendo cha kumsukuma Kijana na kumzuia kuchukua habari na kuwavua fulana baadhi yao ni kitendo cha kidhalili na chakishenzi tunasema sisi kama vijana na wanaharakati tutasimama kidete siku zote katika kusimamia haki na kunyanyua picha za Maulamaa popote tulipo kwani kufanya hivyo kuna baraka kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w.t). Hii ni sms niliyotumiwa na Sheikh kuzuia picha za Maulamaa katika matembezi ya Quds: Salam alaykum, Bwana Ibrahim nakuomba Sana tushirikiane vyema Kwenye matembezi ya Leo na kuwa picha pekee zitakazo ruhusiwa kuonekana ni Zile za viongozi wa kidini na Wala si wa kisiasa, tunafanya hivyo si kwa kuogopa au kutowatambua Bali ni kwa nia ya kuilinda haraka Yetu. Shukran sheikh Ghawth. Hapo kamaanisha Picha za Maulamaa ndio za Kisiasa maana tumeona leo katika matembezi ya Quds zimetawala picha za Mwalimu Nyerere na Mandera hadi mwisho wa matembezi za Maulamaa zimewekwa kando kwa kuhofia kuambiwa wanaunga mkono ugaidi kwa kuwa ugaidi unalelewa na Mwamerika. Astaghafurullah imani yetu ipo wapi enyi ndugu zangu Waislam. Hapa nakumbuka siku Imam Khomein ( R.A) alipokuwa anafanya harakati za kuamsha Ummah aliwaona viongozi wa kidini wakirudi nyuma aliwaita na kuwaambia: Kukaa kimya ni sawa na kuunga mkono dhulma pia alisema: Tekelezeni wajibu wenu katika dini lolote litakalokuwa na liwe.