WAUMINI WA KIISLAM WA MADHEHEBU MBALIMBALI WAMESHIRIKI KATIKA MAZISHI YA CHIEF KADHI MUBARAK.



Mazishi ya Chief Kadhi Mubarak yamefanyika leo Madale Saa 10:00 jion, jijini Dar es Salaam.
Chief Kadhi Mubarak alifariki ghafla majira ya saa kumi na moja Al fajir nyumbani kwake kwa Presha, Chief Kadhi alikuwa ni mmoja wa Wanawarisha wa Kiislam (Waandishi wa Kiislam) na waasisi wa harakati za Kiislam ambao walipigania mafundisho ya Uislam katika Aridhi ya Tanzania na kufanikiwa kusimamisha maamkizi ya Kiislam yani “Assalaam Aleykum” na kuifanya salamu ya kawaida katika jamii yetu hadi sasa na kuleta heshima ya hijabu kwa mwanamke katika jamii ya Kitanzania ambapo hapo mwanzo vazi la hijabu alikuwa na thamani na  maamkizi ya  Kiislam yalikuwa mageni pia walifanikisha kuchapa majalida mbalimbali ya Kiislam yenye lengo la kuelimisha Ummah wa Kiislam na kusimamisha kituo cha kutoa elimu ya Msingi hadi Sekondari kwa ajili ya vijana wa Kiislam kilichopewa jina la Masjid Qubah ambapo ndio kituo Mama na kitovu cha harakati kilichopo Sinza Mori, jijini Dar es Salaam, baadhi ya waasisi wa harakati hiyo wameonyesha masikitiko yao kwa kuondokewa na mtu huyo muhimu ambaye ndio alikuwa nguzo katika kusimamia maendeleo ya harakati hiyo wamesema Chief Kadhi siku zote alikuwa msitari wa mbele katika mambo yeyote na alikuwa mtendaji mzuri katika majukumu yake pia walisema Chief Kadhi katika uhai wake alikuwa mara kwa mara hakiimiza kujitoa katika kusimamia maendeleo ya Ummah bila kusubiri msukumo kutoka kwake, nijukumu letu sote kufuata njia zake . “Tusome Suratul Fatha kwa ajili ya Marehemu wote waliotangulia mbele ya haki”