Waislamu wa Madhehebu ya Shia Ithna Ashariyyah leo wameswali swala ya
Eid Al-Adha kitaifa katika Kiwanja cha Pipo kilichopo Kigogo Post jijini
Dar es Salaam, Khatibu wa Swala ya Eid amewataka Waumini wa Kiislam
kuwa na Taqwa amesema bila ya Taqwa hakuna Uislamu, mambo yeyote katika
jamii ikikosekana Taqwa jamii hiyo haiwezi kufanikiwa pia amesema ni
muhimu Waislam kuwa kitu kimoja kwa kuwa Ibada Tukufu ya Hijjah ni Ibada
inayowakusanya watu bila kuangalia rangi wala makabila kwa hiyo ni
vyema waislam kuungana na kushirikiana katika kila jambo na kuweka mbali
tofauti zao.