WILAYA

Wilaya haukuwa mfumo uliofanywa na Allah Azza wa Jallah kwa ajili ya siku moja au mbili, ulikuwa ni mfumo wa utawala kwa ajili ya Umma baada ya kufariki Mtukufu Mtume (s.a.w.w) mpaka siku ya hukumu. Mfumo huu pia ulikuwepo kabla ya Ghadir na upo palepale daima. Vilevile madhumuni ya kadhia ya Ashura yalikuwa ni kuurudisha Umma kwenye mhimili wa "Wilaya" kwa vile watu walijitenga mbali na Ghadir. Wakati watu wanajitenga mbali na Ghadir, Ashura inajitokeza. Vilevile moyo wa Ashura ni "Wilaya." Wakati watu wanajitenga wenyewe mbali na "Wilaya" walijitumbukiza kwenye Ukhalifa (Khilafat)", na kutoka kwenye "Ukhalifa" mfumo ulibadilika kuwa Ufalme (Mulukiyat), na kutoka kwenye Ufalme ulibadilika kuwa Uyazidi (Yazidiat). Viwango hivi vitatu vya uangukaji chini vilitokea katika jamii baada ya kujitenga mbali na "Wilaya," na Uyazidi (Yazidiat) ulikuwa msiba. Hapo ndipo Ashura ilipokuja na kuwaambia watu kwamba ukombozi wenu upo tu kwenye "Wilaya." Mfumo wa "Wilaya" upo mpaka siku ya hukumu. Hauwezi kusimamishwa kwa kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w) wala kusimamishwa kwa ghaibu ya Maasum (a.t.f.s). Ilikuwa ni uamuzi wa kimungu kwamba Mjumbe (s.a.w.w) lazima afariki. Lazima aende kwenye ghaibu ya kudumu, lakini "Wilaya" ilikuwa hai, ipo na mfumo huu ulikuwepo miongoni mwa Umma. Kama Maasum akienda kwenye hali ya ghaibu kwa mda maalumu, bado mfumo wa "Wilaya" unaendelea kuwepo, na hata kama Maasum akienda nyuma ya mapazia ya ghaibu kwa muda usio na kikomo basi mfumo wa "Wilaya" bado unadumu. Hairuhusiwi sisi kugeuza nyuso zetu mbali na Wilaya ima kwa sababu ya kifo cha Mtume (s.a.w.w) wala kutokana na ghaibu ya Maasum. Na Ustadh Sayyid Jawwad Naqvi