LINI WAPALESTINA WATAKUWA HURU?



Zaidi ya miaka 60 tangu kuanzishwa utawala wa Israel mnamo May, 14, 1948 udhalimu wakina umekuwa ukiendelea. Wakimbizi wa Ki-Palestina ndio idadi kubwa kushida yote ya wakimbizi iliyobakia duniani.
Wapalestina Millioni 1.3 wanaishi nchini Israel kama “Raia wa Israel,” lakini licha ya hadhi yao kama raia, bado wanakumbwa na ubaguzi wa kimfumo hatua kwa hatua. Wengi wao wanakatazwa kuishi kwenye vijiji na makazi yao ambamo walifukuzwa kikatili, na mali zao zimekamatwa kwa ajili ya matumizi ya Kiyahudi tu. Katika Istilahi za Orwellian, sheria za Israel zinawaonyesha wakimbizi hawa wa ndani kama “wasiopo wakati huu” (Present obsentees)
Mnamo mwaka 1967 Israel ilianzisha vita vyake vya tatu na wakatwaa ardhi zaidi ya Wapalestina (na ya Waarabu wengine). Israel pia ilishambulia meli ya kivita ya Marekani, “The USS Liberty,” ikiwauwa na kujeruhi zaidi ya Wamarekani 200, tukio ambalo linabakia kufunikwa kabisa leo hii, licha ya juhudi za kundi lisilo la kawaida la maafisa wa ngazi ya juu wa kijeshi watumishi wa kiraia za kulifichua na kuliweka wazi.
Israel iliukalia Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Gaza asilimia 22 ya mwisho ya mamlaka (iliyokadiriwa) ya Palestina na ikaanza kujenga makazi ya Waisrael wa Kiyahudi kwenye ardhi iliyoporwa kutoka kwa Waislam na Wakristo wa Kipalestina. Imebomoa zaidi ya makazi 24,145 ya Wapalestina tangu mwaka 1967. Mwaka 2005 Israel ilirejesha ardhi ya Gaza kwa wenyewe, lakini inaendelea kudhibiti mipaka yake, bandari na eneo la anga, na kuigeuza Gaza kama gereza kubwa, ambamo watu Million 1.5 wanashikiliwa chini ya kile kinachoelezwa na kamisheni ya haki za Binadamu ya umoja wa Mataifa masharti ya “Kimsiba.”
Zaidi ya Wapelestina 7,000 Wanaume, Wanawake na watoto wamefungwa katika magereza ya Israel chini ya hali ya kudhalilishwa kimwili (Wengi wao wala hawakushitakiwa kwa uhalifu wowote) na haki za msingi za kibinadamu za Wapalestina wote chini ya utawala wa Israel kwa kawaida zikikiukwa. Baadhi ya wafungwa waliopewa mateso na Israel walikuwa ni raia wa Marekani. Katika ukatili ambao ulianza 2000, kupitia Feb. 5, 2009, majeshi ya Israel yaliuwa Wapalestina 6,348; Vikundi vya upinzani vya Palestina viliuwa Waisrael 1,072. Jeshi la Israel, la nne lenye nguvu sana duniani linamiliki mamia ya silaha za nyuklia.