Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Benjamin William Mkapa amesema kuwa, misaada inayotolewa na
madola ya Magharibi kwa nchi za Afrika haina masilahi na
kwamba, lengo la kudhoofisha ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika .Mkapa
amesema kuwa, kuwa mara nyingi nchi za Magharibi zimekuwa zikitoa
misaada kwa masharti ya kutolewa kwa ushuru kwa bidhaa zinazoingia
pamoja na bidhaa zinazouzwa katika mataifa hayo, jambo ambalo linaweza
kudhoofisha ukuaji wa uchumi kwa nchi za Afrika.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesisitiza kwamba, masharti hayo yanapaswa kuepukwa na viongozi wa nchi za Afrika na kusisitiza kwamba hayo yanaweza kuepukika ikiwa mataifa hayo yatawekeza zaidi katika sekta ya elimu kwa kuhakikisha wanawaandaa vijana kwa kuwapatia elimu bora. Benjamin Mkapa alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005. (irib)
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesisitiza kwamba, masharti hayo yanapaswa kuepukwa na viongozi wa nchi za Afrika na kusisitiza kwamba hayo yanaweza kuepukika ikiwa mataifa hayo yatawekeza zaidi katika sekta ya elimu kwa kuhakikisha wanawaandaa vijana kwa kuwapatia elimu bora. Benjamin Mkapa alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005. (irib)