UJUMBE KWA WAUMINI.

Bismillahir Rahmanir Rahim.

Asalaam Aleykum,

Ndugu zetu katika Imani tunapenda kusema kuwa: "Atutorejea nyuma katu katika kuipigania dini ya Mwenyezi Mungu (s.w.t), japo kuwa vikwazo vingi vimetukabili mbele yetu, tunaamini kuwa vikwazo kwetu ndio njia pekee itakayotufanya tufikie malengo yetu katika kuifanikisha kazi ya Allah (s.w.t), pia siku zote katika kuipigania njia ya haki tunaamini kuwa miongoni mwetu watatokea wanafiki na wasaliti, pia ata kunawatakao tumika kwa njia ya siri miongoni mwetu kwa namna yeyote kuharibu Haraka ilimradi zisifikie lengo kuu, kwa hiyo ndugu zetu katika imani tunaitajia sana DUA zenu popote mlipo kwa hali na mali ilituweze kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika kila kona ya inchi yetu., Mwenyezi Mungu (s.w.t) amasema: "Wapo watu miongoni mwa Waumini waliotimiza ahadi waliyoahidiana na Mwenyezi Mungu, baadhi yao wamekwishamaliza nadhiri zao, na wako miongoni mwao wanangojea, wala hawakubadilisha (ahadi yao) hata kidogo." Qur'an: 33:23. "ALLAHUMMA SWALLI A'LAA MUHAMMAD WA A'LAA AALI MUHAMMAD"...