MAULID YA BWA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W), YAMEFANYIKA KATIKA UKUMBI WA DAIMOND JUBILEE,SIKU YA J.PILI

Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, 
alikuwa mgeni rasimi wa Sherehe ya Maulid ya Bwana Mtume Muhammad (s.a.w.w), katika Sherehe hiyo amezungumzia juu ya swala zima la Amani ya inchi ya Tanzania, amesema katika inchi ya Tanzania wanaishi watu mbalimbali wapo watu wenye dini na watu wasio na dini, chamsingi ni kuvumiliana hili kila mmoja wetu haweze kuishi, mwisho kamalizia kwa kuwataka Viongozi wa dini kuamasisha amani pindi wanapokuwa katika majukwaa yao.
 Ummah wa Kiislam umefurika katika ukumbi wa Daimond Jubilee, kwa ajili ya kushereheka juu ya mazazi ya Bwana Mtume Muhammad (s.a.w.w), Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema: "Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika wake humsalia Mtume, enyi mlioamini! msalieni (Mtume) na muombeeni amani." 33:56
 Maulana Sheikh Hemed Jalala, 
Mudir wa Hawzat Al-Imam Swaadiq (a.s), Kigogo Post, Dar es Salaam,(katikati), akiwa katika hali ya furaha baada ya kuona Ummah wa Kiislam ulivyofurika katika ukumbi wa Daimond Jubilee,jijijni Dar es Salaam.
Sayyid Shaheed, 
(katikati) kiongozi wa chuo cha Jamiatul Mustafa University, kilichopo Upanga jijini Dar es Salaam, akiwa katika Sherehe ya Maulid ya Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), yaliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.
 Waumini wa Madhihabu mbalimbali za Kiislam, wakiwa katika Sherehe ya Maulid ya kipenzi cha Mwenyezi Mungu, Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), yaliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam. 
Tarehe: 17-02-213