WILAYA NI MFUMO WA KIMUNGU NA KWA AJILI YA MWONGOZO WA MWANADAMU.


Hawakuweza  kuelewa ile dhati ya “Wilaya” na wakati walipotakiwa kueleza maana yake, walitoa maelezo mepesi sana kama vile “Urafiki” au “Mapenzi.” Je, Mtume (s.a.w.w) baada ya maandalizi yote hayo na ushukaji wa Aya hizo, alikuwa anatangaza urafiki au mapenzi?

Huu ndio wasiwasi uliomshughulisha  Mtume (s.a.w.w) kwamba Ummah unaweza ukaishiliza maana ya “Wilaya” mpaka kwenye urafiki na mapenzi tu, hawatasonga mbele katika kuusimamisha kama mfumo.

“Wilaya” ni mfumo wa Kimungu kwa ajili ya mwongozo wa Wanadamu. Ni mfumo bora sana ambao una khususia (kazi maalum). Sina nafasi ya kuzitaja taaluma za mfumo huu hapa na kuulinganisha na mifumo mingine ya utawala. Hili lilikuwa ni tangazo la mfumo wa utawala wa Kimungu, lakini Ummah hawakuukubali katika njia hii, waliutafsiri kimakosa. Hawa kwenda katika njia ile ambayo Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alitaka waichukue. Hatua ya kwanza waliyochukua ilikuwa ni kujitenga na “Walii” huyo. Wacha ajitokeze yeyote kutokana na “Answar” (Wasaidizi wa Madina) au “Muhajirin” (Wahamiaji kutoka Makka) kuwa kiongozi, lakini Walii wa kweli asijitokeze.

Wilaya haukuwa mfumo uliofanywa na Allah Azza wa Jallah kwa ajili ya siku moja au mbili, ulikuwa ni mfumo wa utawala kwa ajili ya Ummah baada ya kufariki Mtukufu Mtume (s.a.w.w) mpaka siku ya hukumu. Mfumo huu pia ulikuwepo kabla ya Ghadiir na upo palepale daima. Vile vile madhumuni ya kadhia ya Ashura yalikuwa ni kuurudisha Ummah kwenye mhimili wa “Wilaya” kwa vile watu walijitenga mbali na Ghadir. Wakati watu wanajitenga mbali na Ghadir, Ashura inajitokeza. Vile vile moyo wa Ashura ni “Wilaya.” Wakati watu wanapojitenga wenyewe mbali na “Wilaya” walijitumbukiza kwenye Ukhalifa (Khilafat)”, na kutoka kwenye “Ukhalifa” mfumo ulibadilika kuwa Ufalme (Mulukiyat), na kutoka kwenye Ufalme ulibadilika kuwa Uyazidi (Yazidiat). Viwango hivi vitatu vya uangukaji chini vilitokea katika jamii baada ya kujitenga mbali na “Wilaya,” na Uyazidi (Yazidiat) ulikuwa msiba. Hapa ndipo Ashura ilipokuja na kuwaambia watu kwamba ukombozi wenu upo tu kwenye “Wilaya.”

Mfumo wa “Wilaya” upo mpaka siku ya Hukumu. Hauwezi kusimamiswa kwa kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w) wala kusimamishwa kwa ghaibu ya Maasum (a.t.f.s). Ilikuwa ni uamuzi wa Kimungu kwamba Mjumbe (s.a.w.w) lazima afariki. Lazima aende kwenye ghaibu ya kudumu, lakini “Wilaya” ilikuwa hai, ipo na mfumo huu ulikuwepo miongoni mwa Ummah.

Kama Maasum akienda kwenye hali ya ghaibu kwa muda maalumu, bado mfumo wa “Wilaya” unaendelea kuwepo, na hata kama Maasum akienda nyuma ya mapazia ya ghaibu kwa muda usio na kikomo basi pia mfumo wa “Wilaya” bado unadumu. Hairuhusiwi sisi kugeuza nyuso zetu mbali na Wilaya Imma kwa sababu ya kifo cha Mtume (s.a.w.w) wala kutokana na ghaibu ya Maasum. 
Na Sayyid Jawwad Naqvi