SERIKALI YA PALESTINA YATAKA HIMAYA KWA AL-AQSWA.


Serikali halali ya Palestina iliyochaguliwa na wananchi na inayoongozwa na Waziri Mkuu Ismail Haniya imetoa wito wa himaya ya kila upande kwa msikiti mtakatifu wa al-Aqswa. Taher al-Nunu, Msemaji wa serikali ya Palestina amewataka Wapalestina wote wajitokeze na kuuhami msikiti mtakatifu wa al-Aqswa ambao unakabiliwa na hujuma za kila upande za utawala wa Kizayuni wa Israel. Aidha Taher al-Nunu ameutaka umma wote wa Kiarabu na Kiislamu kutekeleza majukumu yao ipasavyo katika kuunga mkono na kuuhami msikiti huo mtakatifu wa al-Aqswa. Msemaji wa serikali halali ya Palestina amesisitiza kwamba, kuna haja ya kuweko himaya ya kila upande na Waislamu wote kwa Masjdul Aqswa, kibla cha kwanza cha Waislamu. Katika siku za hivi karibuni utawala wa Kizayuni umezidisha vitendo vya kuuvunjia heshima msikiti wa Al Aqswa jambo ambalo limewakasirisha Waislamu na wapenda uhuru kote duniani. Utawala huo ghasibu aidha kila Ijumaa huwazuia vijana wa Kipalestina kutekeleza ibada ya Sala ya Ijumaa katika msikiti huo. Habari kutoka http://kiswahili.irib.ir/habari/palestina/item/31937-serikali-ya-palestina-yataka-himaya-kwa-msikiti-wa-al-aqswa