Baadhi ya Waumini wakiwa katika mazishi ya Mwanaharakati wa Madhehebu ya
 Ahlul Bayt (a.s) Bi Subira aliyefariki siku ya J.tano na kuzikwa siku 
ya Alhamisi tarehe 26/02/2015 katika kijiji cha Mtindilo Wilayani 
Lushoto, katika mazishi hayo amehudhuria Sheikh Waziri Nyello aliyekuwa 
Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Ithna Ashariyyah Community (T.I.C). 
Swala ya Jeneza iliongozwa na Sheikh Baqri Mwenda Imam wa Masjid Imam 
Ali bin Abi Talib (a.s) Lushoto. "Hakika sisi sote ni waja wa Mwenyezi 
Mungu na kwake tutarejea" Tusome Suratul Fatha kwa ajili ya ndugu yetu.
