Imam Abu
Shuhadaa Hussein bin Ali (a.s) aliitoa muhanga nafsi yake, ahali zake,
mali zake na vengine vinavyohusiana naye kwa ajili ya Uislamu, hivyo
kuna umuhimu kwa Waislamu kujua mwamko huu Mtukufu kwanza, pili wamuunge
mkono kwa aina zote za msaada na tatu wachukue kigezo kwa Imam
wao katika kujitoa muhanga kwa ajili ya Uislamu. Na Muislamu ajue
kwamba kujitoa muhanga ni katika vitu vinne, na Imam alijitoa muhanga
kwa mambo haya manne katika mapambano ya KARBALA:-
1- Kujitoa muhanga katika nafsi.
2- Kujitoa muhanga katika ahali.
3- kujitoa muhanga katika mali.
4- Kujitoa muhanga katika umaarufu wake.
Imam alijitoa muhanga katika nafsi yake akauliwa. Alijitoa muhanga katika ahali zake mpaka likauliwa kundi miongoni mwao, na wengine wakatekwa. Alijitoa muhanga katika mali zake ambapo aliporwa. Alijitoa muhanga katika umaarufu wake mpaka wakamwita Khawariji na wakamlaani juu ya mimbari. Ni kweli ilikuwa hivyo kwa muda mchache kama ambavyo ni kawaida katika udanganyifu na tuhuma, hivyo ni lazima kwa mwanajihadi asiogope kuvunjika kwa umaarufu wake kama atapigana kwa ajili ya kutengeneza. Kwani Mwenyezi Mungu ndio mwenye kuafiki na kutakwa msaada. Na Muhammad Al - Husayn As - Shirazi
1- Kujitoa muhanga katika nafsi.
2- Kujitoa muhanga katika ahali.
3- kujitoa muhanga katika mali.
4- Kujitoa muhanga katika umaarufu wake.
Imam alijitoa muhanga katika nafsi yake akauliwa. Alijitoa muhanga katika ahali zake mpaka likauliwa kundi miongoni mwao, na wengine wakatekwa. Alijitoa muhanga katika mali zake ambapo aliporwa. Alijitoa muhanga katika umaarufu wake mpaka wakamwita Khawariji na wakamlaani juu ya mimbari. Ni kweli ilikuwa hivyo kwa muda mchache kama ambavyo ni kawaida katika udanganyifu na tuhuma, hivyo ni lazima kwa mwanajihadi asiogope kuvunjika kwa umaarufu wake kama atapigana kwa ajili ya kutengeneza. Kwani Mwenyezi Mungu ndio mwenye kuafiki na kutakwa msaada. Na Muhammad Al - Husayn As - Shirazi