MAADHIMISHO YA KIFO CHA MJUKUU WA MTUME (S.A.W.W) ALIYEUWA KATIKA ARDHI YA KARBALA.

Waumini wa dini ya Kiislam Madhehebu ya Shia Ithna Ashariyyah leo wameazimisha Kitaifa Kifo cha Mjukuu wa Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w) kwa matembezi ya amani yaliyofanyika Kigogo Post, Dar es Salaam. Imam Hussein (a.s) aliuawa katika jangwa la Karbala huko Iraq mnamo mwaka wa 61 Hijjiria kwa ajili ya kupigania haki na utu wa mwanadamu.