SHEIKH TWAHIRU ABDALLAH: MUBALIGHINA WANATAKIWA KUJISHUGHULISHA NA KAZI MBALIMBALI.

Mubalighina hawana budi kufuata nyayo za Sheikh Twahiru Abdallah Imam wa Masjid Al Kisaa na mwalimu wa Madrasa katika Mkoa wa Tanga Wilaya ya Lushoto yeye mbali na kufanya kazi ya kueneza mafundisho sahihi ya dini ya Kiislam katika Wilaya ya Lushoto anajishughulisha na masuala ya kilimo ili kukizi mahitaji yake binafsi na familia yake leo hii imekuwa ni hajabu kuona baadhi ya watu wanafanya kazi ya dini ni sehemu ya kujipatia kipato ili kukizi mahitaji binafsi hii ni njia mbaya Mubalighina anatakiwa kujishughulisha sio katika kazi ya dini tu bali hata kazi binafsi ili haweze kuendesha maisha na harakati kwa ujumla bila ya hivyo kazi ya kuendesha harakati ya dini kila siku itabaki kuwa ni kiini macho bila ya mafanikio jamii inahitaji kuona mfano kutoka kwa watu wa dini hasa katika masuala ya maendeleo Mubalighi wanatakiwa kujitambua kuwa Mubalighi sio maana kukaa bila ya kuwa na shughuli maalumu tunaona hata Maimam wenyewe walikuwa na shughuli za kufanya mbali na kazi ya kuendesha harakati za kidini. Ibnu Abbas anasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa amuonapo mtu na akavutiwa naye, husema: "Je ana kazi?" Wakasema hana, husema: " Hana thamani tena machoni kwangu." Wakamuuliza kwa nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Kwa sababu Muumini asipokuwa na kazi ataishi kupitia dini yake." Rejea: Jamiul - Akhbar: 390/1084.