KWA NINI WATU WENGINE HAWAIKUBALI HII WILAYATUL FAQIIH?

 Kuna sababu nyingi sana nyuma ya hili. Watu wengine ni kutokana na ujinga, wengine kwa shaka za kuundwa, wengine kutokana na sababu nyinginezo na wengine wamepotoshwa na maadui. Kwa maneno mengine, baadhi ya watu wanaposhwa na mawakala wasaliti ambao wamepandikizwa miongoni mwetu ili kuiziba njia hii. Mawakala hawa wanapandikizwa kutokea nyuma na wanapelekwa kwenye mimbari zetu ili kubadili mwelekeo wa jumuiya hii, lengo kuu ni kuukengeusha Umma huu kutoka kwenye mfumo wa maisha wa Kimungu. Ninawasilisha hapa kisa cha kweli kama mfano kwa ajili yako ili upate kuelewa yale yote yaliyofanywa ili kuwapotosha watu kutoka kwenye Wilayatul - Faqiih. Ungeziona na habari pia jana kwamba, ili kubadilisha mfumo wa utawala nchini Syria, Serikali ya Marekani imetenga bajeti ya dola Milioni tano za Kimarekani. Na ili kubadili Serikali nchini Iran Marekani imetenga dola za Kimarekani Milioni ishirini na moja kwa kila mwaka. Pesa hizi wanampa nani? Wanazitoa kwa mawakala kama hawa ambao watakuja kuzungumza dhidi ya mfumo huu wa Wilayat, kuandika chochote na kuendelea kufanya chochote dhidi ya mfumo wa Wilaya. Waliunda baraza huko Marekani kwa jina la UMAA chini ya mwongozo wa Paul Wolfowitz. Huyu Paul Wolfowitz alikuwa ndiye mtaalamu wa ushauri wa mashambulizi ya Marekani huko Iraq. Yeye alibuni shambulizi hili na kisha akalipanga yeye. Chini ya uongozi wake waliunda kamati yenye Ulamaa, Makhatibu wa Kidini na wenye kushikilia mimbari. Lengo la baraza hili ni kufanya kazi kuelekea kwenye kuyasafisha mawazo ya Imam Khomein (R.A) kutoka kwenye Madhehebu ya Shi'ah. Wao walisema kwamba mambo fulani ndani ya Madhehebu ya Shi'ah yameingia kutoka nje na haya ni lazima yaondolewe. Paul Wolfowitz wakati akiwa Mkuu wa Benk ya Dunia alijitokeza kwenye Tv akiwa na sura zinazojulikana sana za watu wa jumuiya ya Shi'ah wakiwa wamekaa pamoja naye. Alisema kwamba mawazo ya Imam Khomein (R.A) yanapaswa kuondolewa kutoka kwenye jumuiya ya Shi'ah. Wametenga Mamilioni ya dola kwa ajili ya shughuli hii. Kwa hiyo sio kwamba kama mtu akikaa kwenye mimbari na kuzungumza dhidi ya Wilaya, basi huo ni uharibifu wa mawazo na akili yake mwenyewe, laahasha. Ukifuatilia mahusiano ya mtu kama huyo yatarudi nyuma mbali kabisa, baadhi ya ofisi za Kibalozi, au NGO fulani zitakuwa nyuma yake huyo. Hivyo inatubidi tuwe na tahadhari na uwerevu. Na Ustadh Sayyid Jawwad Naqvi