"Wala usidhani wale walio uliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa ni
wafu, bali ni hai wanaruzukiwa kwa Mola wao." (Al Imran Aya 169).
Mwezi wa Muharram
upo njiani tuutumie mwezi huu kukuza imani zetu. Karbala inatufunza
maisha namna ya kuishi sio kuomboleza na kula Nihazi tu ni jukumu letu
kuchukua mafunzo ya Karbala na Siku ya Ashura ili tuweze kuishi maisha
bora kama jamii iliyohai na sio jamii ya kitumwa Imam (a.s)
alitoka yeye na kizazi chake na jamaa zake kwa ajili ya kuchukia
udhalili na ukandamizaji dhidi yetu na sisi hatuna budi kuenzi na
kufuata nyayo za watu hawa. Karbala ni
uwanja wa maisha na hii maana yake ni kifo cha Kishahidi. Kifo cha
Kishahidi maana yake ni maisha halisi ya mwanadamu, sio maisha ya kula
nafaka na chakula. Shahidi ameacha vitu vyote hivi lakini bado Allah
anasema anapata riziki. Riziki hii sio chakula kwa ajili ya tumbo lakini
riziki ya maadili, sifa njema na heshima. Shahidi ni yule mtu mwenye
kujiheshimu ambaye hufundisha watu njia ya kuishi maisha. Mshipa wake wa
Shingo hukatwa kwa sababu hataki kuishi kama mnyoo ndani ya mzoga.
Shahidi huzihuisha jumuiya na jumuiya hupata somo la maisha kutoka kwa
Mshahidi. Lakini kama watu wakiogopa baada ya kusikiliza habari za kifo
cha Kishahidi, kwa watu kama hao Allama Iqbal anasema: "Mtu ambaye moyo
wake hutetemeka juu ya habari za kifo cha kafiri ambaye anaweza
kumwambia afe kifo cha Mwislamu, watu kama hao kamwe hawawezi kufa kifo
cha kweli cha mwanadamu na Mwislamu." Na Ustadh Sayyid Jawwad Naqvi