SHEIKH ABDULLATIF SWALEH AMEFANYA ZIARA MKOA WA TANGA WILAYA YA LUSHOTO.

Sheikh Abdullatif Swaleh ametembelea Mkoa wa Tanga, Wilaya ya Lushoto katika msafara wake amebahatika kukutana na Mwanaharakati mkongwe Sheik Waziry Nyello aliyekuwa Mwenyekiti wa Tanzania Ithna Asharyyah Community (T.I.C) yenye makazi yake Kigogo Post, jijini Dar es Salaam, Sheikh Waziry kipindi cha uongozi wake katika taasisi hiyo alisimama kidete kutetea haki za wanyonge na kusimamia maendeleo ya vijana hasa katika upande wa elimu pia alipinga kila aina ya ubaguzi dhidi ya mtu mweusi, alikemea manyanyaso dhidi ya wanyonge kwa wenye nacho katu hakusita kumfuata mtu pindi anapokosea kwa kweli hatuna budi kufuata nyayo zake, Sheikh Abdullatif amesema wilaya ya Lushoto bado ipo nyuma sana kiharakati inaitajika viongozi wake watembelewe mara kwa mara kwa ajili ya kuwatia nguvu ya ufanyaji kazi kwani viongozi hao wamekuwa na malalamiko ya mara kwa mara ya kutopewa ushirikiano baina yao na taasisi nyingine.