SEMINA YA KUJENGA UMOJA BAINA YA WATU WOTE.

Semina ya kujenga umoja na mshikamano baina ya Waislamu na dini zote za mbinguni imefanyika usiku huu wa tarehe 18/06/2014 mjini Posta,jijini Dar es Salaam, Katika Semina hiyo viongozi wa kidini wametakiwa kutoa elimu katika jamii kutokana na matukio yanayoendelea hivi sasa ulimwenguni, viongozi hao wametakiwa kufichua njama dhidi ya makundi haramu yaliyojivisha sura ya Uislamu.