HAWZAT AL-IMAM SWADIQ (A.S) IMEFANYA KUMBUKUMBU YA KUKUMBUKA KIFO CHA IMAM KHOMEIN (R.A).


Kumbukumbu ya kifo cha Imam Khomein (R.A) imefanyika leo katika ukumbi wa Jafarry Complex,jijini Dar es Salaam, karibu na jengo la umoja wavija wa CCM. Imam Khomeini katika uhai wake hakuwahi hata sekunde moja kupuuza jambo lolote katika mikakati ya kuinua jamii ya Kiislamu, hivyo alikuwa Kiongozi wa kisiasa mwenye changamoto na harakati nyingi ulimwenguni. Imam alifariki mnamo tarehe 3/06/1989 usiku siku ya Jumamosi. Imam alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo, sababu iliyopelekea kifo chake ni ugonjwa uliyopatikana kwenye mfumo wa chakula hivyo alilazimika kufanyiwa upasuaji. Imam Khomein wakati wa uhai wake aliamini dharura ya kuwepo mipango, ratiba na udhibiti wa nafsi katika maisha, hivyo alikuwa akitenga muda maalumu usiku na mchana kwa ajili ya ibada, dua, na kisomo cha Qur'an. Alikuwa akishiriki mazoezi ya kutembea huku akimtaja Mwenyezi Mungu na kufikiria mustakbali, kiasi kwamba alifanya kufikiria mustakbali ni sehemu ya ratiba yake ya kila siku. Pamoja na kuwa na kazi nyingi na mikutano ya mara kwa mara na viongozi wa utawala wa Kiislamu lakini suala la kukutana na watu wa kawaida alilipa umuhimu wa pekee, hivyo aliendelea na ratiba yake ya kila wiki ya kukutana na familia za mashahidi hadi siku za mwisho za maisha yake. "KUMUENZI IMAM KHOMEIN NI KUFUATA NJIA YAKE."