MAREKANI YACHUKIZWA NA MAFANIKIO YA JESHI LA SYRIA.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiU6j1npE1jpoF7lD6_Pm9pONx3-0IykMnxh3_p-96zH9L25RWPD_22Xq-6ZX9EI0CovYUymts6QtpyFa-Uv02SzdtSf9_PygdGlblYhpBXQSg9lmrKz9zx2D_dwjyWSFcUcTShkjIHM3Y/s640/Jasusi.jpg)
Seneta wa chama cha upinzani cha Republicans
nchini Marekani, John McCain ameelezea kuchukizwa kwake na mafanikio ya
jeshi la Syria dhidi ya makundi ya kigaidi yanayoungwa mkono na Washington na waitifaki wake.
McCain ameiambia kanali ya televisheni ya CBS kwamba serikali ya Rais
Barack Obama inafaa kuingilia kati mara moja la sivyo, Rais Bashar al
Assad atazima kabisa nguvu za magaidi hao na kwamba hilo litakuwa pigo
kubwa kwa ikulu ya White House.
Wiki iliyopita, seneta huyo
aliingia kinyemela huko Syria na kukutana na viongozi wa makundi ya
waasi wenye silaha, jambo lililodhihirisha wazi uhusiano uliopo kati ya
Marekani na makundi hayo ya kigaidi.
Huku hayo yakijiri, habari
zinasema kuwa jeshi la Syria limeendelea na oparesheni kali za kuwasaka
magaidi katika mji wa Qusayr na kwamba magaidi kadhaa wa kundi la
Jabhat an-Nusra wameuawa.
Kwa upande mwingine magaidi wa Syria
wamejaribu kumuua kamanda mmoja wa harakati ya Hizbullah kwa madai
kwamba harakati hiyo inamsaidia Rais Bashar Asad. Watu wenye silaha
wamefyatulia risasi gari la kamanda huyo ingawa hawakufanikiwa kumuua au
hata kumjeruhi.