IRAN NI MSHIKA BENDERA YA UMOJA WA KIISLAM.


Mkuu wa Baraza la Kidini la Hizbullah nchini Lebanon amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni mshika bendera wa umoja na mshikamano wa Kiislamu ulimwenguni. Sheikh Muhammad Yazbek ameongeza kuwa, Iran kwa kuunga mkono kadhia ya Palestina imeweza kuonyesha kivitendo umoja na mshikamano wa Waislamu na kusisitiza kuwa jambo lolote linalozungumzwa kinyume na uhakika huo, litakuwa ni katika mwendelezo wa mikakati na njama chafu za Marekani na waitifaki wake katika eneo za kuichafua Iran. Sheikh Yazbek ameongeza kuwa, kama madola ya kibeberu ya Magharibi yataacha uungaji mkono wao kwa makundi ya magaidi nchini Syria, wananchi wa nchi hiyo  wataweza kutatua mgogoro  uliopo kwa njia ya mazungumzo. Mkuu wa Baraza la Kidini la Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, iwapo serikali ya Rais Bashar al Assad itapinduliwa huko Syria basi jambo hilo litabadilisha kabisa mustakbali wa Wapalestina na kadhia nzima ya Palestina ulimwenguni. 
Habari kutoka http://kiswahili.irib.ir/habari/iran/item/31444-iran-ni-mshika-bendera-ya-umoja-wa-kiislamu