Sheikh
 Hemedi Jalala Kiongozi wa Chuo cha dini ya  Kiislam Kigogo Post, Dar es
 Salaam, amekutana na viongozi wa Msikiti wa Mtambani uliyopo Kinondoni 
jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujadiliana juu ya changamoto 
mbalimbali zinazowakumba waislamu ndani na Nje ya Nchi. Mazungumzo yana 
lengo la kuwakutanisha viongozi wa dini tukufu ya Kiislamu katika meza 
moja na kujaribu kutizama changamoto zinazoukabili uislamu ikiwemo 
hatari ya Makundi ya kukufurishana na Ugaidi yanayokithiri kuibuka kila 
uchao. Aidha mazungumzo yanalengo kutafuta njia za kuwaunganisha 
Waislamu na kuwa na sauti moja katika masuala yanayowaunganisha dhidi ya
 Maadui zao.
