Mkuu wa Shirika la Hija na Umra la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema 
kuwa kuna uwezekano wa kufutwa safari zote za ndege za Wairani 
wanaokwenda Saudia Arabia kwa ajili ya ibada ya Umra.
 Hatua hiyo 
imekuja baada ya askari wawili wa Saudia kuwadhalilisha kijinsia 
mahujaji wawili vijana wa Kiirani katika uwanja wa ndege wa Jeddah 
waliokuwa wakirejea nyumbani baada ya 
kukamilisha ibada ya Umra. Kwa kutumia kisingizio cha kuwapekua vijana 
hao, askari wawili wa Saudia walifikia hatua ya kutaka kuwanajisi lakini
 mahujaji wenzao walichukua hatua za haraka za kutoa taarifa 
zilizopelekea kukamatwa askari hao wawili.
Mkuu wa Shirika la Hija na Umra la Iran amemtaka Waziri wa Hija wa Saudia, Bandar bin Muhammad kuwafungulia mashtaka na kuwachukulia hatua kali askari hao wahalifu ili kurejesha imani na utulivu wa kiroho kwa mahujaji wa Iran wanaokwenda nchini humo kwa ajili ya ibada za Hija na Umra.
Mkuu wa Shirika la Hija na Umra la Iran amemtaka Waziri wa Hija wa Saudia, Bandar bin Muhammad kuwafungulia mashtaka na kuwachukulia hatua kali askari hao wahalifu ili kurejesha imani na utulivu wa kiroho kwa mahujaji wa Iran wanaokwenda nchini humo kwa ajili ya ibada za Hija na Umra.
