UDHALILI HAUTAKIWI KWA MWANADAMU.

Hii inatuonyesha ya kuwa Udhalili hautakiwi kwa Mwanadamu kwa kuhofia vikwazo na vitisho kutoka kwa wenye nguvu, mwanadamu anatakiwa kusimama imara siku zote katika kupambana na dhulma, ukandamizaji pamoja na unyanyasaji dhidi ya mwanadamu kukaa kimya ni sawa na kuunga mkono dhulma . Hapa ni muhimu sana tukumbuke maneno ya mjukuu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alipotoka pamoja na familia yake na Masahaba zake kuelekea katika ardhi ya Karbala kwa ajili ya kujitolea Muhanga maisha yao kwa ajili ya kuchunga heshima na Utukufu wa mwanadamu. Imam Hussein (a.s) alisema: "Daima udhalili ni mwiko kwetu"