SEMINA YA MUBALIGHINA YAFANYIKA BILAL MUSLIM MISSION TEMEKE, JIJINI DAR ES SALAAM.


Taasisi ya Bilal Muslim Mission imeandaa Semina fupi ya siku mbili kwa Mubalighina wanaofanya kazi ya kueneza mafundisho sahihi ya Uislam wa Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w) Semina hiyo imeanza siku ya J.nne ya tarehe 06/05/2014 Bilal Temeke, jijini Dar es Salaam, katika Semina hiyo wameshiriki Masheikh na Walimu wa dini kutoka sehemu mbalimbali Lushoto,Rufiji Ikwiriri, Kondoa, Mtwara Arusha, Moshi, n.k katika Semina hiyo wameudhuria takribani watu 40 Semina inatarajia kumalizika siku ya Jumatano tarehe 07/05/2014.