WAUMINI WA DINI YA KIISLAM WAUNGANA MASJID GHADIIR, KIGOGO POST, JIJINI DAR ES SALAAM, KUSHEREHEKEA MAZAZI YA IMAM ALI BIN ABI TALIB (A.S).

Mwalimu wa Hawzat Al-Imam Swaadiq (a.s), Sheikh Said Othaman, amewahutubia Waumini wa dini ya Kiislam leo katika Masjid Ghadiir, Kigogo Post, Da re Salaam, amewataka Waumini hao kuwa na Umoja na Mshikamano baina yao, pia amesema Waislam hawanabudi kuyafuata mafundisho ya Imam Ali bin Abi Talib (a.s), na kuangalia jinsi gani alivyoweza kuishi na jamii.
 
Baadhi ya Waumini wakiwa katika Sherehe ya Mazazi ya Imam Ali bin Abi Talib (a.s), iliyofanyika leo Masjid Ghadiir, Kigogo Post, jijini Dar es Salaam, Sherehe hiyo iliongozwa na Sheikh Said Othaman Mwalimu wa Hawzat Al-Imam Swaadiq (a.s), iliyopo Kigogo Post, Dar es Salaam.

 Waumini wa Madhehebu mbalimbali ya Kiislam leo wameungana Masjid Ghadiir, Kigogo Post, jijini Dar es Salaam, kusherehekea Mazazi ya Imam Ali bin Abi Talib (a.s), katika picha Waumini hao wakisoma Dua ya Umoja na mshikamano baina ya Waislam.