SHEIKH PONDA ISSA PONDA, KATIBU WA JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAM, TANZANIA, AMEHUKUMIWA KIFUNGO CHA NJE CHA MWAKA MMOJA.


Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam,
 ametoa hukumu ya kifungo cha nje cha mwaka mmoja kwa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, huku akiwaachia huru wafuasi wake 49 waliokuwa wamejumuishwa kwenye kesi yake. Kwa mujibu wa duru za Tanzania, Sheikh Ponda na wenzake walikuwa wanakabiliwa na mashtaka matano likiwemo la uchochezi. Awali Wakili wa Utetezi, Juma Nassoro akitoa hoja za majumuisho mbele ya Hakimu Victoria Nongwa aliiomba Mahakama iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu, kwa kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kujenga kesi na kuthibitisha tuhuma dhidi ya washitakiwa.