MKUTANO WA ‘MAULAMAA NA MWAMKO WA KIISLAMU’ KUFANYIKA TEHRAN.


Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
 imeandaa kongamano la kimataifa la ‘Maulamaa na Mwamko wa Kiislamu’ ambalo litafanyika Tehran wiki ijayo.
Akizungumza na waandishi wa  habari hii leo, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Mwamko wa Kiislamu Dk Ali Akbar Velayati amesema kuwa, kongamano hilo ambalo litafanyika Jumatatu na Jumanne wiki ijayo litawaleta pamoja Maulamaa 500 wa kigeni na 200 kutoka hapa nchini Iran.
Dk Velayati amesema, kongamano hilo litachunguza matatizo ya nchi za Kiislamu na vile vile changamoto zilizopo katika harakati za Mwamko wa Kiislamu. Aidha ameashiria njama za maadui za kuibua vita vya kimadhehebu nchini Syria na kusema maadui wameanzisha njama hizo baada ya kushindwa kuvunja muqawama nchini humo. Amesema maadui hao wa Uislamu watafeli katika njama zao za kuibua vita vya kimadhehebu nchini Syria. Velayati amesema, Iran inapinga harakati za Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu na kieneo dhidi ya Syria. Amesema Iran inazihesabu njama hizo dhidi ya Syria kuwa ni chuki na uadui dhidi ya Waislamu. Kutoka http://kiswahili.irib.ir/habari/habari/item/31370-mkutano-wa-%E2%80%98maulamaa-na-mwamko-wa-kiislamu%E2%80%99-kufanyika-tehran