Mtume Muhammad (s.a.w.w) amesema: "Enyi watu, 
hakika mimi nawatangulia nanyi mtanikuta katika haudhi. Fahamuni kuwa 
mimi nitawauliza kuhusu vizito viwili, hivyo angalieni jinsi gani 
mtahusika navyo baada yangu. Hakika Mpole mtoa habari amenipa habari 
kuwa: Hakika hivyo viwili havitoachana mpaka vinikute. Nilimuomba Mola 
wangu hivyo na akanipa. Fahamuni hakika mimi nimewaachieni Kitabu cha 
Mwenyezi Mungu na Kizazi changu Ahlul-Bayt, hivyo msiwatangulie 
mtafarikiana, wala msiwaache mtaangamia 
na wala msiwafunze hakika wao ni wajuzi zaidi yenu. Enyi watu! Msiwe 
makafiri baada yangu ikawa baadhi yenu wanawauwa wengine hivyo mkanikuta
 huku mkiwa kundi dogo kama mfereji wa maji uliyoacha njia. Fahamuni 
kuwa Ali bin Abi Talib ni ndugu yangu na wasii wangu, atapigania Tafsiri
 ya Qur'an baada yangu kama nilivyopigania uteremkaji wake."
 
Rejea: Tarikh Yaaqubiy, Juz. 2 Uk. 109
Rejea: Tarikh Yaaqubiy, Juz. 2 Uk. 109
